
wajameni awali ya yote niombe radhi kuwa siku za hivi karibuni blogu yenu pendwa imekuwa na kwikwi mara kwa mara, hii ni kutokana na sababu zilizo nje kabisa ya uwezo wangu, lakini yote ni majaaliwa yake jalali, inshallah yatakwisha na hali itarejea kama hapo kabla, kwa sasa naomba niwasalimu tu kwani nagonjeka, afya imeleta mgogoro kidogo, tuvute subra nitarejea kumwaga uhondo kwenu wadau.