Monday, December 5, 2011

TUTAKUKUMBUKA DAIMA!

HALI YANGU YAENDELEA VEMA!


Baada ya kufanyiwa upasuajikwa mara ya pili JOSE MARA mwanamuziki wa kundi la mapacha watatu amesema anaendelea vizuri na karibuni atarudi jukwaani.

Thursday, December 1, 2011

PATCHO MWAMBA "TAJIRI" MUZIKI HADI FILAMU


kama ilivyo kwa wasanii wakubwa ulaya na amerika ndivyo patco mwamba mwanamuziki toka FM ACADEMIA anaonekana kwa sasa akitesa katika medani ya filamu za kibongo na mwenyewe anasema anafurahi kujua kuwa ana kipaji kingine ambacho ni kama amechelewa kukijua.

KEVIN MOLA! UJIO MPYA AFRIKA!



Wadau kimya kingi kina mshindo mkuu, na hivi ndo taratibu narejea.

Sunday, November 7, 2010

JUMAPILI YA MARAFIKI!


Hakuna kitu poa kama baada kazi nyingi kupata tym ya kurelax na kuenjoy na marafiki, my very best friend carol magessa (wa pili kushoto) akila bata na marafiki.

Thursday, October 28, 2010

HAYA WADAU MPANGO UKO HIVI!


Picha mbili zinazoonyesha matangazo ya wanamuziki wawili na ziara zao jijini paris, tayari washabiki wa damu wa muziki wa Congo wameanza kutupa maoni yao juu ya ushindani usoisha wa wakali hawa wa Congo wakiufananisha upinzani wao na ule wa jb mpiana na werrason, haya mdau nimerudi mzigoni kaa nami ujue nini kitatokea huko paris wakati hapa bongo sie mwezi ujao tutamwona live fally ipupa kwa mara ya pili kama mwanamuziki wa kujitegemea.

Monday, October 25, 2010

FERRE NA FALLY VITA MPYA UFARANSA!



katika kile kinachotafsiriwa kuwa ni mwendelezo wa vita ya kimuziki kati yao wanamuziki matata wa congo FALLY IPUPA na FERRE GOLA wanatarajiwa kuwa katika vita ya kufungua mwaka jijini paris, wakati fally anadai ziara yake ilipangwa na kutangazwa mapema waratib wa ziara ya ferre wameingilia mpango huo na kutaka kutibua hali ya hewa kwa wapenzi wa muziki huo waliojaa nchini ufaransa.

Wednesday, June 9, 2010

ITS BIG DAY FOR BIG JOE!


ni zaidi ya boss, zaidi ya rafiki, leo ni hakika siku muhimu kwako. i pray to the most high akupe kila lililo jema katika yote ufanyayo, happy birthday joseph kussaga. pichani aonekana akipiga story na msanii 50 cent alipozuru nchini.

Saturday, March 27, 2010

NIMEWAMIS MNO NDUGU ZANGU!


wajameni awali ya yote niombe radhi kuwa siku za hivi karibuni blogu yenu pendwa imekuwa na kwikwi mara kwa mara, hii ni kutokana na sababu zilizo nje kabisa ya uwezo wangu, lakini yote ni majaaliwa yake jalali, inshallah yatakwisha na hali itarejea kama hapo kabla, kwa sasa naomba niwasalimu tu kwani nagonjeka, afya imeleta mgogoro kidogo, tuvute subra nitarejea kumwaga uhondo kwenu wadau.

Wednesday, March 17, 2010

HAPPY BIRTHDAY CAPTAIN GARDNER G HABASH


ni hakika unaposherehekea siku yako ya kuzaliwa nyuma yako tuko wengi uliotuvutia hadi kufikia hatua tuliyonayo leo, hongera sana brother gardner g habash.

Wednesday, March 10, 2010

TSHALA MWANA AWA MBOGO!



malkia wa mutuashi Tshala Mwana amechukizwa vikali na kuondoka ukumbini kwa hasira baada ya tuzo aliyotarajia ya msanii bora wa kike kwa sauti "best female voice award" kutunukiwa barbara kanam, na akasikika akibwabwaja " laiti ningesikiza ushauri wa koffi na wengine,,," sijui ni ushauri gani alipewa na akakaidi, haya tena ndo mambo ya muziki hayo. ikumbukwe album ya KARIBU ya barbara kanam inatesa sana kwa wasanii wa kike wa congo kwa sasa.

Monday, March 8, 2010

NI WERASON NA MBWEMBWE ZA CONCERT YA ZENITH!


katika kile kionekenacho kama jamaa kadhamiria kuandika historia mpya katika onyesho la paris werasson sasa anasema unaweza kujishindia tiketi na album ya techno malewa kwa ajili ya onesho hilo la tar 13 march zenith, kama nawe kama mie ingia hapa www.afrozic.com

Friday, March 5, 2010

NI ZAMU YA KUWA TIMAMU!


ulimwengu wa teknohama unazidi kukua kwa spidi ya kasi ya ajabu, hapa nina raha kumtambulisha mblogishaji aliye timamu kitimamu. mtembelee hapa upate yaliyo timamu. http://timamusana.blogspot.com/

NYOTA NDOGO ATIMIZA NDOTO ZA UTANGAZAJI!


mwishoni mwa mwaka jana msanii toka mombasa kenya alitarajia kuanza kazi yake mpya ya utangazaji lakini mambo yakaenda kombo,hivi sasa upepo unamwendea vema diva huyo kwani tangu jumatatu ya tar 1 march anaruka hewani katika kituo cha radio ya BARAKA FM, na mwenyewe anasema "ni ndoto iliyotimia naahidi sitawaangusha mashabiki wangu" huyo ndo nyota ndogo muziki hadi utangazaji.

MNAMKUMBUKA YONDO SISTER?


wadau leo nimemkumbuka sana mwanamuziki huyu ambaye historia yake imegubikwa na vituko, haya wenye kumbukumbu na mbwembwe zake mwageni data wana wa afrika tuenjoy.

JB MPIANA KUFA NA KUPONA MWAKA HUU!


pichani anaonekana JB MPIANA katika onyesho maalum aliloliita ST VALENTIN 2010, mpiana yuko jikoni akiandaa album mpya inayokwenda kwa jina la Aller Soyons Serieux
akimaanisha "Let's be serious" yani tuwe makini, nadhani ni baada ya kutofanya vizuri kwa album yake iliyopita huku hasimu wake mkubwa werason akingara na album yake ya techno malewa.

Monday, March 1, 2010

TSHALA MUANA NA TUZO "SANTURI YA DHAHABU"


malkia wa mutuashi Tshala Muana anatarajiwa kutua jijini paris kukabithiwa tuzo ya "santuri ya dhahabu" (gold disc) baada ya mauzo album yake ya "sikila" kuuza zaidi ya nakala 140,000,malkia huyo wa mutuashi amealikwa na kampuni inayosimamia kazi yake ili akabidhiwe tuzo yake hiyo.