Labda "akutendeaye mabaya" ndiye akujaliye!!!!
21 hours ago
si ajabu katika hafla mbalimbali kuwaona viongozi wetu wakiserebuka na wanamuziki wetu, lakini utamu wa hii ni kwamba mh mohamed dewji mbunge wa singida mjini (ccm) aliamua kupanda jukwaani kabisa na kwenda sambamba na wanenguaji wa bendi ya twanga pepeta, halafu hebu cheki hilo snepu ni kama braza mzoefu vile? kama vipi wabunge waanzishe bendi yao jamani tupate uhondo.
sio ndoto wala hadithi za kufikirika MOPAO KOFFI OLOMIDE katika sherehe za miaka 22 ya L’orchestre Quartier Latin International amedhamiria kwaalika wanamuziki wote waliopitia katika band yake. tukio hilo litafanyika jumamosi ya november 28 ndani ya Grand hotel jijini kinshasa. katika list ya walioalikwa majina kama fally ipupa na ferre golla yapo kwenye v.i.p list. haya bwana huyo ndio koffi bwana, tusubiri kuona nini kitatokea na kama ada nitawapa vipande hapahapa kunako VIVA. papaa joe mutu ya zenji upoooo.
Ile ziara ya mwanamuziki Ras Nas aka Nasibu Mwanukuzi katika miji sita ya Norway karibu inamalizika. Hapa ni kwenye ukumbi wa MS Innvik, Oslo, ambapo Ras Nas na kikosi chake waliwasha moto mkali usiku wa Halloween; Jumamosi iliyopita. Hivi sasa Ras Nas amejipanga kufyatua CD ya muziki na mashairi "Double Focus". Mashairi yanatoka kwenye kitabu ambacho Nasibu aliandika mwaka 1989 pamoja na shairi moja la Shabaan Roberts “Titi la Mama”. Kwa hiyo hivi sasa kaa chonjo!picha na habari kwa hisani ya Wadau wa Kongoi Productions http://www.kongoi.com/
tume ya maadili inaposhangilia namna isiyofurahisha ya uchezaji kwa madensa wao, lakini hivi sasa congo uvaaji na staili ya uchezaji ni mjadala mkubwa, hapa kwetu basata waliwahi kutishia kuzifungia bendi za dansi ambazo wanenguaji wake wanavaa bila kuzingatia maadili, haya ngoja tuone nini kitafuata katika mjadala huu.
ilikua ni kama hadithi na sasa mambo yanamweneda kombo mopao koffi oliomide, jamaa anakabiliwa na mashitaka ya ubakaji na huenda akahukumiwa na mahakama ya ufaransa ambako kesi hiyo inaunguruma. kwa mujibu wa taarifa miaka miwili iliyopita akiwa katika ziara ya kimuziki nchini huko alikua na wacheza show wake wakiwemo mabiti 4 wenye umri kati ya miaka 14 na 17 na kwa mujibu wa sheria hilo ni kinyume cha sheria, koffi anadaiwa kuwafungia wasichana hao ndani chini ya ulinzi mkali na kazi yao ni kumrisha kimapenzi anapowahitaji, haya kama mjuavyo hapa viva hapakauki mambo endelea kuwa nami ntakupa kitakachojiri.
msanii toka mombasa kenya Mwanaisha Abdalla a.k.a Nyota Ndogo yu mbioni kuanza kazi ya utangazaji hivi karibuni. nyota anawindwa na kituo cha Baraka FM ili ajiunge na timu hiyo. mapaparazi walimfumania nyota katika jengo la Cannon Towers zilipo ofisi za Baraka FM ambako yasemekana anapata mafunzo ya RADIO. taarifa zimezidi kumwagika kuwa mkali huyo atakuwa akiendesha kipindi kimoja mwisho wa wiki kitakachoanza kuruka mwishoni mwa mwaka. NZULA MAKOSI ndiye mwalimu wa nyota kuendesha vifaa vya studio. "ni kweli napata mafunzo hayo, lakini mmepata wapi taarifa hizo?" alihoji nyota ndogo.
vijana walioitumikia kwa mafanikio makubwa "Quartier Latin Internationale" ya KOFFI OLOMIDE, soleil wanga, fally ipupa, na ferre gola ambao wote sasa wanafanya kazi kama wasanii wa kujitegemea na tayari album zao ziko sokoni. haya wadau pedeshee ndama, papaa musofe"chuma cha reli", big producer maghambo, abdull tall, bila kumsahau pius mikongoti nipeni data nani mkali hapa.
mwaka 2002 koffi olomide na papa wemba walitoa album ya "wake up" na hivi karibuni papa wemba alitoa malalamiko kuwa koffi hakufanya sawa katika mapato ya album hiyo sasa limeibuka jipya, aliyekuwa mzalishaji mkuu wa album hiyo coco rubenga katika mtandao wa intaneti ametangaza kuwa anamdai koffi kiasi cha $ 120,000 ambazo ni sawa na euro 80,000 ambazo alifanya kazi katika album hiyo.